Watu 17 wauawa shambulizi la hoteli
Watu
walioshuhudia wamenukuliwa wakisema kwamba, watu watatu waliokuwa na bunduki
waliwafyatulia risasi wateja waliokuwa nje ya hoteli moja na mgahawa.
Eneo
la katikati mwa jiji limezingirwa na maofisa wa jeshi na ubalozi wa Marekani
mjini hapa, umewatahadharisha raia wake wasiende eneo hilo.
Watu
30 waliuawa katika shambulio la kijihadi katika mgahawa mdogo ulio karibu na mji
huu mnamo Januari mwaka jana.
Kuna
wasiwasi kwamba, shambulio hilo huenda limetekelezwa na moja ya washirika wa
mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda ambao bado wanaendesha shughuli zao katika eneo
la Sahel.
Waziri
wa Mawasiliano nchini, Remis Dandjinou amesema haijabainika ni washambuliaji
wangapi hasa waliohusika.
“Wamejibanza
katika sehemu moja ya jumba waliloshambulia. Maofisa wa usalama wanaendesha
oparesheni ya kuwafurusha,” alisema kwenye televisheni.
Ufyatuaji
wa risasi ulianza muda mfupi majira ya usiku wa kuamkia leo, katika barabara
yenye shughuli nyingi ya Kwame Nkrumah. Maeneo mawili, Hotel Bravia na Aziz
Istanbul Restaurant, yanaonekana kulengwa na washambuliaji.
“Shambulio
lilisababisha vifo vya watu 17, ambao uraia wake bado haujathibitishwa, na
wanane wamejeruhiwa,” taarifa ya Serikali iliyonukuliwa na shirika la habari la
AFP inasema.
Hospitali
moja mjini humu, ilisema mmoja wa waliouawa ni raia wa Uturuki.
Shambulio
hilo linakaribiana sana na shambulio lililotekelezwa Januari 2016, ambapo watu
wenye silaha walishambulia hoteli ya Splendid Hotel na mgahawa wa karibu wa
Cappucino, pia katika barabara ya Kwame Nkrumah Avenue.
Watu
zaidi ya 170 walishikwa mateka na 30 wakauawa. Al-Qaeda walikiri kuhusika.
Burkina
Faso inapatikana katika eneo la Sahel, ambalo linajumuisha pia nchi ya Mali
ambapo makundi ya Kiislamu yamekuwa yakitekeleza mashambulio tangu mwaka 2012.
BBC
No comments