Asubuhi Njema; Morata kutua Chelsea # Liverpool yampandia Keita # Man United wamfuata Verratti
LONDON- CHELSEA wamefikia
makubaliano na Real Madrid, kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wao, Alvaro
Morata (24) kwa dau lenye thamani ya pauni milioni 70 (sh bilioni 203).
Timu hiyo pia imeripotiwa kutaka dau la pauni
milioni 44 (sh bilioni 127.6), kutoka Atletico Madrid kama ada ya kumuuza Diego
Costa. Hata hivyo, Rais wa Atletico Madrid, Enrique Cerezo amesema hawezi kutoa
kiasi hicho. Independent.
Liverpool iko tayari kutoa pauni milioni 70 (sh
bilioni 203), kama dau la kumsajili kiungo wa RB Leipzig ya Ujerumani, Naby
Keita. Dau hilo linakuja baada ya dau lao la pili la pauni milioni 66
kukataliwa. Mirror.
Manchester United imejitosa mazima kwenye dili la
kumsajili kiungo wa PSG ya Ufaransa, Marco Verratti (24) baada ya Muitaliano
huyo kuingia mkataba na Mino Raiola ili awe wakala wake. Sun.
West Ham wanatarajiwa kumsainisha muda wowote
mshambuliaji wa Bayer Leverkusen, Javier Hernandez (29), kwa dau ambalo
linadaiwa kuwa pauni milioni 13 (sh bilioni 37.7). Sky Sports.
Man
United wanafuatilia kwa karibu hatima ya kiungo wa Everton, Ross Barkley (23)
klabuni hapo, lakini wanatarajiwa kugonga mwamba kwani Barkley mwenyewe amesema
anahitaji kujiunga na Tottenham Hotspurs. Standard.
Wakongwe
wa soka la Italia, AC Milan, wamesema kuwa mshambuliaji wao, Suso (23) ambaye
anawindwa vikali na Tottenham Hotspurs, hauzwi. Talksport.
Inter
Milan imewaambia Man United kuwa, dili lolote lenye nia ya kumtaka winga wao,
Ivan Perisic (28) lazima limhusishe mshambuliaji Mfaransa, Anthony Martial (21)
pamoja na pauni milioni 48 (sh bilioni 139.2). Independent.
Imebainika
kuwa Manchester United na Chelsea zilikuwa zikifukuzia kimya kimya dili la
kumsajili mshambuliaji wa Barcelona, Neymar (25) lakini walikwamishwa na
kifungu kinachodai kuwa thamani ya mchezaji huyo ni pauni milioni 196 (sh
bilioni 565.5). Mail.
Newcastle
wamekubali ombi la Everton, ambao walikuwa wakimhitaji kinda wao Lewis Gibson
(17). Everton wanataka beki huyo ajiunge na kikosi chao cha wachezaji wa under
23. Liverpool Echo.
No comments