Picha mbalimbali za Mtanzania aitwaye Nelson Issangya anayejishughulisha na utunishaji misuli nchini Marekani.
Licha ya kujishughulisha na utunishaji misuli, pia ni mtaalam wa sayansi ya kompyuta kwa ngazi ya shahada.
Anasema tangu mwaka 2015 amekuwa akishiriki katika
mashindano mbalimbali ya Bodybuilding (utunishaji misuli) ambapo huwa anashindana
kwenye category mbili, Bodybuilding na Classic Physique.
Mashindano ambayo ameshiriki na kushinda yote ni
NPC Oregon State Championships, NPC Cascadian Classic ambako alishinda mara mbili
na May 27, 2017 atashindana tena katika shindano hilo.
Pia ameshinda kwenye shindano kubwa ambalo
linajulikana kama NPC Emerald Cup. Baada ya shindano hilo la May 27, 2017 atajiandaa
kwa shindano lingine kubwa la NPC USA Championships ambalo litafanyika July
2018 mjini Las Vegas.
No comments