Asubuhi njema; Bakayoko kutua muda wowote Chelsea # Mourinho amtaka Dier wa Spurs # Wenger kumbakiza Sanchez
LONDON-
KWA mujibu wa vyanzo vya kuaminika vya Sky Sports, Chelsea wapo karibu zaidi
kumsainisha kiungo wa Monaco, Tiemoue Bakayoko (22) na muda wowote ataweza
kutua London kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya.
Bakayoko
anatarajiwa kufanyiwa vipimo hivyo na kusafiri na timu kwenda Singapore,
Jumatatu ijayo. Inadaiwa kuwa dau lililokubaliwa ni kati ya pauni milioni 35-40
(sh bilioni 101 au 120). Sky Sports.
Kocha
wa Manchester United, Jose Mourinho, ameutaka uongozi wa klabu hiyo kupeleka
dau la pauni milioni 60 (sh bilioni 174) kwa Tottenham Hotspurs ili kumsajili
kiungo wao, Eric Dier (23). Mirror.
Kocha
wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa anategemea ataendelea kupata huduma ya
mchezaji wake, Alexis Sanchez (28) ambaye bado hajakubali kusaini mkataba mpya
na klabu hiyo kutokana na kudaiwa kutaka kuhamia Manchester City. Independent.
Manchester
United bado hawajafikia makubaliano rasmi na Inter Milan, kuhusiana na usajili
wa Ivan Perisic (28), lakini dili hilo linalodaiwa kuwa ni pauni milioni 50 (sh
bilioni 145) linatarajiwa kukamilika muda wowote wiki ijayo. Independent.
Arsenal
wanadaiwa kujitosa rasmi kwenye mpambano wa kumnyakua beki wa kati wa
Southampton, Virgil van Dijk (26) ambaye anatakiwa na klabu za Liverpool na
Manchester City. The Sun.
Roma
ya Italia imeweka wazi mpango wao wa kumtaka kwa mkopo wa msimu mzima
mshambuliaji wa Man United, Anthony Martial (21) lakini United hailitaki dili
hilo. Mirror.
James
Rodriguez ameiambia Real Madrid kuwa anataka ajue mustakabali wa maisha yake ya
soka klabuni hapo, kutokana na kutakiwa na Man United na Chelsea. Hata hivyo,
inadaiwa Madrid wanataka pauni milioni 62 () kama ada yake. Daily Mail.
Leicester
City wamekubaliana na Man City kuhusu vigezo vya msingi bya usajili wa
mshambuliaji wao kinda, Kelechi Iheneacho (20), lakini haijawekwa wazi ni kiasi
gani wamewapatia wababe hao wa Manchester. Sky
Sports.
Licha
ya kuendelea kubakia katika viwanja vya mazoezi vya Carrington, Manchester,
akielekea kupona maumivu ya goti, Zlatan Ibrahimovic bado hajapewa mkataba na
Man United wamedaiwa kutokuwa tayari kumwongezea mkataba mshambuliji huyo. Star.
Manchester
City imedaiwa kuwa ni moja kati ya klabu nne za Ulaya, ambazo ziko tayari
kulipa pauni milioni 27 (sh bilioni 78.3) kama ada ya uhamisho ya mshambuliaji
wa Real Sociedad, Inigo Mrtinez (26). Marca.
No comments