Asubuhi Njema; Bakayoko kusaini miaka 5 Chelsea # Arsenal watoa £45 kwa Lemar # Matic aitaka United # Hazard awaita Madrid
LONDON- Chelsea wamefikia makubaliano na klabu ya Monaco, kuhusu usajili
wa kiungo wao, Tiemoue Bakayoko (22), kwa dau la pauni milioni 40 (sh bilioni 116).
Bakayoko atasaini mkataba wa miaka 5 muda wowote kuanzia sasa. RMC.
Klabu ya Arsenal, inaamini kuwa ofa yao ya pauni milioni 45 (sh bilioni 130.5)
ni nzuri na wanatarajia kuwa itakubaliwa na Monaco, kwa ajili ya uhamisho wa
winga Thomas Lemar. Daily Mail.
Chelsea wameelezwa kwamba, wanaweza kumsajili mshambuliaji wa Borussia
Dortmund, Piere-Emerick Aubameyang kwa ada ya pauni milioni 60 (sh bilioni 174),
baada ya miamba ya soka la China, Tianjin Quanjian kujitoa kwenye usajili wa
mchezaji huyo mwenye miaka 28. Daily Mail.
Baada ya kuona kuwa straika wao mkali, Piere-Emerick Aubameyang anaweza
kuondoka muda wowote, Borussia Dortmund wamejitosa kwenye mchakato wa kumsajili
Olivier Giroud wa Arsenal, ambaye pia anatakiwa na West Ham. Daily Mail.
Winga wa Chelsea, Eden Hazard (26) amemtaka kocha wa Real Madrid,
Zinedine Zidane kuamua kuhusu hatima ya usajili wake kwenda kwa mabingwa hao wa
Ulaya msimu huu. Daily Express.
Mchezaji wa zamani wa Liverpool, Danny Murphy, amesema klabu hiyo iko
mbioni kukamilisha usajili wa mlinzi wa kati wa Southampton, Virgil van Dijk
(26) kwa dau ambalo halijawekwa wazi. Sport360.
Baada ya kufanikiwa kumpata kiungo wa Monaco, Tiemoue Bakayoko, sasa
kocha wa Chelsea, Antonio Conte, anatarajiwa kumuweka sokoni kiungo
wake,Nemanja Matic. Mserbia huyo amekuwa akifanya mazoezi peke yake na anadaiwa
kusema kuwa anataka aungane na Jose Mourinho huko Man United. Daily Telegraph.
Chelsea wanatarajiwa kuipiku Juventus kwenye usajili wa beki, Danilo
kutoka Real Madrid kwa dau la pauni milioni 28 (sh bilioni 81.2). Daily
Miror.
No comments