Header Ads

Watoto 30 wafariki kwa kukosa hewa India



https://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/story_large/public/thumbnails/image/2017/08/12/19/an128047524topshot-editor.jpg

UTTAR PRADESH- WATOTO wachanga 30 wamefariki dunia katika hospitali moja jimboni hapa, baada ya kukosa hewa ya oksijeni ambayo ilikuwa ikiwasaidia kupumua.
Upungufu wa hewa hiyo muhimu kwa vichanga vilivyozaliwa kabla ya muda, ulitokana na hospitali hiyo kudaiwa fedha nyingi na wazabuni wanaosambaza bidhaa hiyo hospitalini hapo.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani nchini, aliliambia shirika la habari la Press Trust la India kuwa, ni watoto 21 ndiyo waliofariki kutokana na tatizo hilo la ukosefu wa hewa ilhali wengine walifariki kutokana na vifo vya kawaida.
Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, matenki ya kutunzia hewa hiyo yaliishiwa oksijeni na kusababisha vifo hivyo na kusababisha matabibu kuanza kuwapatia wazazi mabegi maalum ya kupumulia ili kuwaokoa watoto wao.
“Tulishuhudia watoto waliokuwa wakituzunguka wakipoteza maisha. Kwa kawaida, ni kosa la hospitali. Watoto wengi walifariki dunia kwa sababu ya uzembe wao. Mwanangu alikuwa mzima hadi kufikia usiku, wakati tuko baya lilipomfika,” alisema mmoja wa wazazi ambaye alijitambulisha kwa jina la Vijay.
Independent.

No comments

Powered by Blogger.