Jioni Njema; RB Leipzig waigomea Liverpool # Man City waipiga bao Chelsea # Conte kocha ghali zaidi Chelsea
LEIPZIG- DAU lenye thamani ya pauni milioni 66 (sh
bilioni 191.4) kutoka Liverpool, limekataliwa na klabu ya RB Leipzig ya mjini
hapa ikiwa ni usajili wa kiungo Naby Keita. RB Leipzig wanadai kiungo huyo
hauzwi. Times.
Sky Sport
Italia imeeleza kuwa Manchester
City imeipiku Chelsea, kwenye mbio za kumsajili beki wa Real Madrid, Danilo
(26) kwa dau la pauni milioni 31 (sh bilioni 89.9).
Antonio Conte, amekuwa kocha wa kwanza kulipwa fedha nyingi katika
historia ya Chelsea baada ya kusaini mkataba mpya ambao utamfanya alipwe pauni
milioni 9.5 (sh bilioni 27.5) kwa mwaka. Evening Standard.
Kiungo wa Liverpool, Kevin Stewart (23) amerudishwa Uingereza kutoka Hong
Kong kwa ajili ya kukamilisha dili lake la kujiunga na Hull City kwa dau lenye
thamani ya pauni milioni 8 (sh bilioni 23.2). Liverpool Echo.
Mlinda mlango wa West Ham United, Darren Randolph (30) anaweza akajiunga
na Newcastle United, baada ya wagonga nyundo hao wa London kumsajili kwa mkopo
kipa wa Man City, Joe Hart. Chronicle.
Kocha wa Stoke City, Mark Hughes amejitosa kwenye mchakato wa kumuwania
winga wa Schalke 04, Yevhen Konoplyanka (27), kama mbadala wa Marko Arnautovic
ambaye amejiunga na West Ham United. Stoke Sentinel.
No comments