Kagame aapishwa urais Rwanda
Katika
sherehe hizo zilizofanyika jana katika uwanja wa taifa wa Amahoro jijini hapa,
marais 20 kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika walifika na kushuhudia shughuli
hiyo ya uapishaji.
Kuapishwa
kwa Kagame, kunafuatia ushindi alioupata katika uchaguzi uliofanyika mwishoni
mwa Julai, ambapo alipata ushindi wa asilimia 98 ya kura zote zilizopigwa na
kuwaacha mbali wapinzani wake, Philippe Mpayimana na Frank Babineza waliopata
asilimia 1 ya kura zote.
Kwa
upande wa viongozi wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Kenya
iliwakilishwa na Rais Uhuru Kenyatta ambaye naye alishinda uchaguzi wa urais
kwa kupata asilimia 54 dhidi ya 44 za Raila Odinga.
Uganda
iliwakilishwa na Rais Yoweri Museveni, huku taifa jipya katika jumuiya hiyo ya
EAC, Sudan Kusini likiwakilishwa na Rais wake, Salva Kiir, huku Rais wa
Burundi, Pierre Nkurunziza akishindwa kuhudhuria sherehe hizo kwa sababu ambazo
hazikuwekwa wazi.
Tanzania
iliwakilishwa na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ambaye
alihudhuria kwa uapishaji huo kwa niaba ya Rais wa sasa, Dk John Magufuli.
Aidha,
sherehe hizo zilihudhuriwa na marais wastaafu wa mataifa ya Afrika wakiongozwa
na Olusegun Obasanjo kutoka Nigeria, pamoja na Festus Moghae wa Botswana.
No comments