Modric aionya Real Madrid kwa Rodriguez # Chlesea yatoa £70m kwa Morata # Sanchez na Bellerin waondolewa ‘list’ ya Arsenal
MANCHESTER- KIUNGO Mshambuliaji wa Real
Madris, Luka Modric amesema
kitendo cha klabu hiyo kutaka kumuachia mshambuliaji wake, James Rodriguez
kujiunga na Manchester United kitakuwa ni kosa kubwa.
Mcolombia huyo amekuwa akiitaka Real Madrid imwache akatafute timu
nyingine ambayo atakuwa na uhakika wa kuwepo kwenye kikosi cha kwanza na
kucheza mara kwa mara.
Chelsea wanapanga kutoa kitita cha pauni milioni 70 (sh bilioni 203),
kama ada ya uhamisho wa mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro Morata.
Hayo yanajiri muda mfupi, baada ya Man United kuwapora windo lao kutoka
Everton, Romelu Lukaku. Morata amekuwa akitakiwa kwa muda mrefu na Man United
na hivyo kuilazimu Chelsea kuongeza umakini kwenye usajili wake, ili wasije
wakaporwa tena.
Licha ya kuwepo kwa habari kuhusu mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa kutotakiwa
na kocha wa timu hiyo, Antonio Conte kwenye kikosi chake, mchezaji huyo ni
miongoni mwa wachezaji wanaotarajiwa kurejea mazoezini leo.
Straika huyo alisema hivi karibuni kwamba, Conte alimtumia ujumbe mfupi
wa maneno (sms) ukimjulisha kuwa hatakiwi tena klabuni hapo licha ya kufunga
magoli 20 msimu uliopita na kuisaidia timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya
Uingereza.
Kikosi cha timu ya Arsenal, kimeruka kwenda Australia kwenye ziara bila
ya wachezaji wake wawili, Alexis Sanchez na Hector Bellerin ambao wameongezewa
muda wa kupumzika.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa wachezaji hao wanabaki ili kukamilisha madili
yao ya usajili. Pia, wachezaji wapya wawili, Alexandre Lacazzette na Sead
Kolasinac, wanatarajiwa kucheza michezo yao ya kwanza na timu yao mpya.
Windo la klabu ya Barcelona, Paulinho, amedaiwa kueleza kuwa atakutana
na Rais wa klabu yake ya Guangzhou Evergrande ili kufanya mazungumzo
yatakayomuwezesha kuondoka klabuni hapo na kujiunga na wababe hao wa Hispania.
Habari zote na Sky Sports
No comments