Asubuhi Njema; Mbappe ateta saa tatu na Wenger # Dier aitaka United # Barkley shakani Everton
LONDON- MSHAMBULIAJI kinda wa Monaco na Ufaransa, Kylian Mbappe (18)
anadaiwa kufanya mkutano wa saa tatu na kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ambao
umejadili uwezekano wa mchezaji huyo kujiunga na Arsenal. Express.
Kiungo wa Tottenham Hotspurs, Eric Dier amesema anahitaji kuondoka
klabuni hapo na kujiunga na Man United. United wanatarajiwa kutoa pauni milioni
50 (sh bilioni 145) kwa ajili ya kuinasa saini ya mchezaji huyo. Guardian.
Hatima ya kiungo mshambuliaji wa Everton, Ross Barkley imezidi kuingia
utata kutokana na kocha wa timu hiyo, Ronald Koeman kumuondoa kwenye orodha ya
wachezaji walioenda Tanzania. Daily
Mail.
Wababe wa jiji la Manchester, Manchester United wameanza mazungumzo ya mkataba
mpya na kiungo wao mahiri, Ander Herrera (27) ambayo yatasababisha alipwe pauni
175,000 (sh milioni 507.5) kwa wiki. Daily
Star.
Klabu ya Everton, inahitaji kuziba pengo la Romelu Lukaku kwa kumsajili
mshambuliaji wa Crystal Palace, Christian Benteke, lakini Palace wanaonekana
kuwa wagumu kumuuza mchezaji huyo ghali zaidi klabuni hapo. Daily Mirror.
Man United wanatarajiwa kumuongezea mkataba wa mwaka mmoja mshambuliaji
wao, Zlatan Ibrahimovic (35), hapo Oktoba atakapokuwa amepona majeraha yake. Sun.
Lucas Leiva wa Liverpool anatarajiwa kukamilisha muda wowote usajili
wake Lazio, baada ya majogoo hao wa Anfield kutompa ofay a mkataba mpya
mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30. Daily
Star.
Atletico Madrid wameongeza juhudi zao za kumsajili mshambuliaji wa
Chelsea, Diego Costa, baada ya kuyakosa mawindo yao matatu. Pia, timu hiyo iko
kwenye mchakato wa kumsajili mchezaji wa Monaco, Fabinho ambaye anatakiwa na
Man United. Independent.
PSG wanadaiwa kumtaka beki wa Manchester City na Ufaransa, Eliaqim
Mangala. ESPN.
Winga wa klabu ya Bayern Munich, Douglas Costa (26), amewasili jijini
Turin, kwa ajili ya kukamilisha dili lake la kuhamia Juventus. ESPN.
Kwingineko, PSG iko karibu kabisa kumsajili beki wa Brazil, Dani Alves (34)
bure, baada ya kukatisha mkataba wake na Juventus. Awali Alves alikuwa
akitakiwa kwa ukaribu na Man City. Telegraph.
No comments