Asubuhi njema; Man Utd ‘kuifanyizia’ tena Chelsea kwa Bakayoko # Arsenal watoa pauni milioni 45 kwa Lemar # Szczesny kujiunga na Juventus
LONDON- Baada ya kukamilisha dili la kumsainisha Romelu Lukaku na kuipiku
Chelsea, Manchester United wanatarajiwa ‘kuteka’ tena windo la Chelsea kutoka
Monaco, Tiemoue Bakayoko (22) baada ya kukubali kutoa pauni milioni 35 (sh
bilioni 101.5). Daily Star.
Baada ya Wayne Rooney kurudi nyumbani, Everton sasa wameweka mezani dau
la pauni milioni 32 (sh bilioni 92.8), kwa ajili ya kumsajili kiungo wa Swansea
City, Gylfi Sigurdsson (27). Daily Mail.
Arsenal wako tayari kurudi kwa mara ya tatu kwa Monaco na kutoa dau la
pauni milioni 45 (sh bilioni 130.5), kwa ajili ya kumsajili winga wao, Thomas
Lemar, baada ya dau lao la kwanza na la pili kukataliwa. Daily Mail.
Mlinda mlango wa Arsenal, Wojciech Szczesny (27), ameondolewa katika
orodha ya wachezaji watakaoelekea kwenye ziara ya Australia, ili aweze
kukamilisha uhamisho wake wa kuelekea Juventus. The Sun.
Newcastle United wako mbioni kukamilisha dili lenye thamani ya pauni
milioni 8.5 (sh bilioni 24.6), kwa ajili ya kumsajili kiungo wa Norwich, Jacob
Murphy (22) licha ya kutakiwa na timu za Southampton na Cystal Palace. Daily
Mirror.
Middlesbrough wanatarajiwa kukamilisha dili la kumsajili kwa mkopo winga wa Liverpool, Sheyi Ojo (20) kwa ajili
ya kuitumikia klabu hiyo msimu ujao. Times.
No comments