Header Ads

Wabaya wangu walitaka kuniua - Zuma



https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/16015/production/_97333109_jacobzumaa.jpg

CAPE TOWN- RAIS Jacob Zuma amebainisha kwamba, wabaya wake walijaribu kumuua kwa sumu kutokana na msimamo wake wa kufanya marekebisho ya umiliki wa ardhi na kiuchumi.
Rais Zuma aliyabainisha hayo Jumapili mwishoni mwa wiki iliyopita, alipokuwa akihutubia mkutano wa chama chake cha African National Congress (ANC) mjini KwaZulu Natal.
“Niliwekewa sumu ambayo ilikaribia kuniua, kwa sababu Afrika Kusini ilijiunga na Muungano wa Brics unaounganisha mataifa ya Brazil, Urusi, India, China na jamii ya kibiashara ya Afrika Kusini chini ya uongozi wangu.
“Walisema nilikuwa nina mpango wa kuharibu nchi,” alisema Zuma.
Akihutubia mkutano wa wanachama wa ANC huko Phongolo, Kwa Zulu Natal uliofanyika Jumapili, Zuma alisema alilengwa alipotaka kuweka marekebisho makali ya kiuchumi.
Kulingana na ripoti hiyo, kulikuwa na majaribio matatu ya kumuua. Hata hivyo, Zuma hakusema ni nani aliyejaribu kumuua lakini anasema ni mtu wake wa karibu.
BBC

No comments

Powered by Blogger.