Header Ads

Raila kuanika namna alivyoibwa kura leo



https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/A0AD/production/_97333114_railaz.jpg

NAIROBI- KIONGOZI wa upinzani nchinI, Raila Odinga ambaye alishindwa katika uchaguzi wa urais uliopita, ameliambia gazeti la Financial Times la Uingereza kwamba leo atafichua ushahidi kuhusu namna alivyoibiwa kura.
“Tutauonyesha ulimwengu wote, namna mfumo ulivyochezewa,” alisema Raila.
Raila ambaye alikuwa akiwania urais kwa mara ya nne, alibainisha kwamba hatowania tena urais na kuwataka Wakenya kujua kilichofanyika wakati wa uchaguzi huo.
“Sio suala la kuwa mbifasi, sio suala kuhusu Raila Odinga, sitawania urais tena......tunataka Wakenya kujua kile kilichofanyika, na kile ambacho ulimwengu haujui kinafanyika,” alisema Raila.
Raila amedai kwamba, wadukuzi waliingilia kompyuta za tume ya Uchaguzi na kuweka hesabu ambazo zilimpatia ushindi rais Uhuru Kenyatta. Hata hivyo, madai hayo yamepuuzwa na tume ya uchaguzi.
BBC

No comments

Powered by Blogger.