Header Ads

Maporomoko ya mlima na mafuriko yaua watu 300 Sierra Leone



https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/13135/production/_97333187_b1955443-6d5d-4dc8-bba7-cda5f2298596.jpg

FREE TOWN- WATU zaidi ya 300 wanahofiwa kupoteza maisha, kutokana na maporomoko ya udongo na mafuriko mjini hapa, na huenda idadi hiyo ikaendelea kuongezeka.
Inahofiwa kwamba, miili zaidi ya watu waliofariki dunia kutokana majanga hayo, iko chini ya vifusi. Jitihada za uokoaji, zilisitishwa kwa muda baada ya giza kuingia.
Rais Ernest Bai Koroma amesema kupitia televisheni ya taifa kwamba, vituo vya dharura vimewekwa ili kukabiliana na kile alichokiita janga la taifa.
Shirika la Msabala mwekundu, limesema inakadiriwa zaidi ya watu 300,000 wamepoteza makazi.
Eneo lililoathirika zaidi ni wilaya ya Regent, iliyopo pembezoni Freetown baada ya mlima uliojaa maji kuporomoka.
BBC

No comments

Powered by Blogger.