UN yakataa ombi la Raila kuchunguza matokeo ya uchaguzi Kenya

NAIROBI- UMOJA
wa Mataifa (UN), umekataa ombi la kiongozi wa upinzani nchini, Raila Odinga
kukagua matokeo ya uchaguzi wa Agosti 8, mwaka huu.
Msemaji wa UN,
alikataa ombi hilo akisisitiza taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio
Gutierrez ambayo amewataka viongozi wa Kenya kusuluhisha mgogoro wowote wa
uchaguzi huo katika taasisi zinazofaa Kikatiba.
UN imesema
kuwa utatazama mpango mpya wa Raila, ambao anapanga kutangazwa leo.
Wiki iliyopita,
kiongozi huyo wa NASA alitoa mwito kwa Umoja wa Mataifa kukagua matokeo hayo ya
uchaguzi uliokamilika.
Akizungumza
na gazeti la Financial Times, Raila alisema kuwa ana ushahidi wa
kuthibitisha kwamba uchaguzi huo wa urais ulifanyiwa udanganyifu.
“Tutauonesha
ulimwengo ule mchezo uliochezwa. Kile tunachotaka ni Umoja wa Mataifa kubuni
jopo la wataalam, ambalo litatusaidia kutathmini matokeo hayo,” alisema Raila.
Kiongozi
huyo wa upinzani alisema kuwa, IEBC ilikuwa chini ya shinikizo kali kutoka kwa
maofisa wa Serikali inayoongozwa na Rais Kenyatta.
“Kufuatia
mauaji ya mtaalam wa masuala ya kiteknolojia katika tume hiyo Chris Msando,
wafanyakazi wengine waliogopa.
“Kile
kilichotokea kimeshinikizwa na Serikali. Siyo kuhusu mimi na wala si kuhusu
Raila Odinga kutokuwa mgombea tena. Tunataka Wakenya kujua kilichofanyika, kile
ambacho dunia nzima haielewi kinafanyika.
“Hakuna haja
ya watu kwenda kupanga milolongo mirefu ya kupiga kura kwa saa kadhaa, ama
kufanya kampeni na huku kompyuta moja katika tume ya IEBC inatumiwa kuchakachua
matokeo hayo,” alisema Raila.
BBC
No comments