Kiongozi wa upinzani Zambia aachiwa huru

LUSAKA- KIONGOZI
wa upinzani nchini, Hakainde Hichilema ambaye anakabiliwa na mashataka ya
uhaini ameachiliwa huru, kwa mujibu wa chama chake.
Hichilema
alikamatwa Aprili mwaka huu, baada kudaiwa kuhatarisha maisha ya Rais Edgar
Lungu kwa kukataa kuupisha msafara wa Rais Edgar Lungu wakati viongozi hao wakielekea
kwenye sherehe za kitamaduni Magharibi mwa nchi.
Kiongozi
huyo wa chama cha UPND pamoja na wafuasi wake watano, walifunguliwa mashtaka ya
uhaini, ambayo ni makosa yasiyokuwa na dhamana kwa kulingana na sheria za
Zambia. Walikana mashtaka hayo.
Taarifa zilieleza
mapema kuwa kuachiliwa kwake ni sehemu ya makubaliano yaliyoongozwa na Jumuiya
ya Madola.
Katibu Mkuu
wa jumuiya hiyo, Patricia Scotland, alikuwa nchini wiki iliyopita ambapo
alikutana na Rais Lungu na Hichilema. Baadaye alisema kuwa, Hichilema
ataachiliwa kwa manufaa ya nchi.
BBC
No comments