Asubuhi Leo; Chelsea wamtaka Belotti # Arsenal kukataa ofa za Sanchez # Juventus wamtaka Fellaini
LONDON- CHELSEA wanadaiwa kuanza kumuwinda mshambuliaji wa
Torino ya Italia, Andrea Belotti lakini bado haijawekwa wazi wameweka dau lenye
thamani gani. Belotti anatakiwa ili azibe pengo la Diego Costa. Daily Star.
Kocha wa
Arsenal, Arsene Wenger amesema klab hiyo itakataa ofa yoyote itakayoletwa na
timu yoyote kama ada za uhamisho za Alexis Sanchez na Alex Oxlade-Chamberlain. Wenger
anatarajia wachezaji hao wataheshimu mikataba yao. Daily Mirror.
Liverpool imeiambia
Barcelona kwamba, ofa yoyote kutoka kwa wababe hao wa Hispania yenye nia ya kumnunua
Philippe Coutinho ni lazima ihusishe uwepo wa kiungo Ivan Rakitic. Daily
Express.
Klabu ya
Juventus ya Italia, imemuorodhesha kiungo wa Manchester United, Marouane
Fellaini kama mchezaji namba moja kati ya wengi wanaotakiwa na mabingwa hao wa
Serie A. Sun.
Jaribio la
Chelsea kutaka kumsajili beki wa Juventus, Alex Sandro, limegonga mwamba baada
ya wababe hao wa Ligi Kuu ya Italia kukataa ofa iliyowasilishwa na mabingwa wenzao
kutoka Uingereza. Daily Mail.
Kiungo Mfaransa
anayekipiga Inter Milan, Geoffrey Kondogbia, ameambiwa afanye mazoezi peke yake
kufuatia kukwaruzana na uongozi wake. Kondogbia anawindwa na Liverpool na
Tottenham. Talksport.

Kocha wa
Chelsea, Antonio Conte amemtaka Diego Costa awasilishe barua ya kuomba kuuzwa
klabuni hapo. Tayari timu hiyo inadaiwa kuzipiga chini ofa mbili zenye thamani
ya pauni milioni 52 (sh bilioni 150.8) na pauni milioni 61 (sh bilioni 176.9). London Evening Standard.
Tottenham
wanadaiwa kufikia makubaliano na beki wa PSG, Serge Aurier. Awali mchezaji huyo
alidaiwa kukubaliana maslahi binafsi na Man United, lakini kibali cha kuingia
Uingereza kilizua utata. L’Equipe.
Chelsea imehamishia
akili zao, kwenye mpango wa kumsajili beki wa Southampto, Cedric Soares, wakati
timu hiyo ikijaribu kusajili wachezaji kadhaa ili kuimarisha kikosi chao kwenye
dirisha hili kubwa. Telegraph.
Mazungumzo baina
ya West Ham na Sporting Lisbon yamekwama, kutokana na timu hizo kutoafikiana kuhusu
ada ya usajili wa William Carvalho. Sporting wanataka pauni milioni 40 (sh
bilioni 116). Sun.
No comments