Header Ads

Ulinzi waimarishwa Bomas Kenya



http://www.the-star.co.ke/sites/default/files/styles/new_full_content/public/1614546.jpg?itok=DZn2N5NY

NAIROBI- ULINZI umeimarishwa katika eneo la Bomas ambalo Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC), imekuwa ikilitumia kuandaa na kutangaza matokeo ya uchaguzi uliofanyika kote nchini Agosti 8.
Hali hiyo inakuja, ikiwa ni IEBC inatarajiwa kutangaza rasmi matokeo ya urais muda wowote kuanzia sasa.
Leo asubuhi, IEBC ilipokea jumla ya fomu 270 kati ya 290 za 34b, na inaendelea kusubiri fomu 20 za aina hiyo ambazo zinatarajiwa kuwasilishwa muda wowote hapo Bomas.
Tume hiyo imesema kuwa, mara baada ya fomu hizo zilizobaki kuwasili na kuhakikiwa na maofisa wa IEBC na mawakala wa wagombea, ndipo itatangaza rasmi matokeo ya urais ambayo yamekuwa yakisubiriwa.
Awali, NASA ambao ni Muungano wa Upinzani nchini, ilidai kuwa mfumo wa uchakataji matokeo wa IEBC ulidukuliwa na wadukuzi ambao walipindua kura za Raila Odinga.
Pia, NASA waliitaka tume hiyo kumtangaza Raila kuwa ndiye mshindi kutokana na kudai kuwa alipata kura nyingi zaidi ya mpinzani wake, Rais Uhuru Kenyatta wa Jubilee.
Hata hivyo, madai hayo ya NASA yalitupiliwa mbali na Mwenyekiti wa IEBC, Wefula Chebukati ambaye alidai kuwa wadukuzi hawakufanikiwa kudukua mfumo huo licha ya kujaribu kufanya hivyo.
The Standard Digital.

No comments

Powered by Blogger.