Header Ads

Coutinho kuikosa Watford kesho



https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/01/632277292.jpg?w=620&h=444&crop=1

LIVERPOOL- LIVERPOOL wanatarajiwa kucheza mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu (EPL) kesho, kwa kuwakabili Watford bila ya kiungo wao mahiri, Philippe Coutinho ambaye ana maumivu ya mgongo.
Majogoo hao wa Anfield, wataikosa huduma ya mchezaji huyo baada ya daktari wa timu hiyo kuthibitisha kuwa ana maumivu ya mgongo ambayo yanatarajiwa kumuweka nje kwa muda ambao hakuutaja.
Coutinho, amekuwa nguzo muhimu kwa Liverpool na kocha Jurgen Klopp ambaye amekataa kata kata kumuuza kwenda Barcelona licha ya kupewa dau la pauni milioni 100 (sh bilioni 290).
Sky Sports.

No comments

Powered by Blogger.