Header Ads

Arsenal na Leicester City kukata utepe EPL leo



http://sporteology.com/wp-content/uploads/2017/07/Arsenal-v-Leicester-City-1.jpg

LONDON- MCHEZO wa kwanza wa Ligi Kuu nchini maarufu EPL, unatarajiwa kuchezwa leo ambapo Arsenal watakuwa katika uwanja wao wa nyumbani Emirates, kuwakaribisha Leicester City.
Mchezo huo unaotarajiwa kuanza majira ya saa 9:45 kwa saa za Afrika Mashariki, utakuwa mkali kutokana na namna timu hizo zinavyokuwa na upinzani.
Arsenal ambao wamewasajili Alexandre Lacazette na Sead Kolasinac, wanatarajiwa kuingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu za kushinda mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Chelsea kwa penati baada ya kutoka sare ya 1-1 katika dakika 90 za mchezo.
Vikosi vinatarajiwa kuwa kama ifuatavyo;
Arsenal; Petr Cech, Rob Holding, Per Mertesacker, Nacho Monreal, Hector Bellerin, Granit Xhaka, Mohamed Elneny, Alex Iwobi, Alexandre Lacazette na Danny Welbeck. Arsenal watatumia mfumo wa 3-4-3
Leicester City; Kasper Schmeichel, Danny Simpson, Wes Morgan, Harry Maguire, Christian Fuchs, Mathew James, Onyinye Ndidi, Riyad Mahrez, Shinji Okazaki, Marc Albrighton na Jamie Vardy. Mfumo wao unatarajiwa kuwa 4-2-3-1.

Utabiri wangu
Mchezo wa leo unaweza ukaisha kwa Arsenal kuibuka na ushindi wa bao 2-1.

No comments

Powered by Blogger.