Header Ads

Trump amshukuru Putin kwa kufukuza wafanyakazi wa ubalozi



https://ichef-1.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/C419/production/_96910205_mediaitem96910204.jpg

WASHINGTON DC- RAIS Donald Trump amemshukuru Rais wa Urusi, Vladimir Putin kwa kuagiza kuondoka kwa wafanyakazi 755 kutoka kwenye Ofisi za Ubalozi wa Marekani nchini Urusi.
Akizungumza na wanahabari mjini New Jersey, Rais Trump alisema angependa kumshukuru kiongozi huyo wa Urusi kwa kuisaidia Marekani kuokoa fedha.
Uchunguzi unafanyika nchini kubaini iwapo kulikuwa na ushirikiano kati ya maofisa wa kampeni wa Trump na Urusi, inayodaiwa kuingilia uchaguzi mkuu wa mwaka 2016. Trump ameushutumu uchunguzi huo.
Mwishoni mwa Julai mwaka huu, Rais Putin alisema wafanyakazi 755 wangelazimishwa kuondoka kutoka ofisi za kibalozi za Marekani nchini Urusi, akilipiza kisasi hatua ya Marekani kuiwekea Urusi vikwazo zaidi.
Wengi wa wafanyakazi hao ni waajiriwa kutoka Urusi, ikiwa na maana kwamba watu ambao watalazimishwa kuondoka nchini humo hawafiki 755.
Alisema watatakiwa kuondoka kufikia Septemba 1 mwaka huu, na kufanya idadi ya wafanyakazi katika ofisi za kibalozi wa Marekani kuwa 455, sawa na wafanyakazi wa kibalozi wa Urusi walio Washington.
Wafanyakazi katika ubalozi wa Marekani mjini Moscow, pamoja na ofisi za kibalozi katika miji ya Ekaterinburg, Vladivostok na St Petersburg wameathiriwa.
Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Nje nchini ilitaja hatua hiyo kuwa ya kusikitisha na isiyofaa. Lakini Trump amemshukuru Putin kwa kupunguza wafanyakazi wanaolipwa mishahara na Serikali ya Marekani.
“Ningependa kumshukuru kwa sababu tunajaribu kupunguza wafanyakazi wetu, na kwangu mimi namshukuru kwamba amewafukuza watu wengi kiasi hicho,” alisema.
Aidha, Rais Trump alisema jana kuwa alishangazwa na uvamizi uliofanywa na maofisa wa uchunguzi nchini katika nyumba ya mwenyekiti wa zamani wa kampeni zake, Paul Manafort iliyopo Virginia.
Mwanasheria maalum, Robert Mueller, anayeongoza uchunguzi kuhusu tuhuma kwamba Marekani iliingilia uchaguzi wa Urusi, aliondoka nyumbani kwa Manafort mjini Alexandria akiwa na ‘nyaraka kadhaa’ kwa mujibu wa gazeti la Washington Post.
BBC


No comments

Powered by Blogger.