Header Ads

Mwenyekiti IEBC asema matokeo ya wapinzani hayaeleweki



https://3dwnh01icn0h133s00sokwo1-wpengine.netdna-ssl.com/wp-content/uploads/2017/06/Chebukati-IEBC.jpg

NAIROBI- MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC), Wafula Chebukati amesema tume hiyo ilipokea barua kutoka kwa muungano wa upinzani (NASA) ambapo wanadai mgombea wao Raila Odinga ndiye aliyeshinda uchaguzi mkuu uliofanyika Jumanne.
Chebukati amesema matokeo hayo hayaeleweki, kwa sababu muungano huo haukuambatanisha Fomu 34A za matokeo vituoni ambazo walitumia kufanya hesabu yao.
Aidha, ameongeza kuwa muungano huo unafanya makosa kwani ni kinyume cha sheria kwao kujitangazia matokeo.
Hadi sasa, matokeo ya awali yanaonesha Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee anaongoza akiwa na kura 8,163,572 dhidi ya kura 6,747,099 za Raila Odinga wa chama cha ODM kilicho katika muungano wa National Super Alliance maarufu NASA.
Matokeo yaliyotangazwa ni ya vituo 40489 kati ya vituo 40883. Kura zilizoharibika zimeendelea kuwa nyingi, na kufikia sasa ni kura 399 935.
BBC

No comments

Powered by Blogger.