Header Ads

Asubuhi Leo; Barcelona wakwama Dortmund # Real Madrid wateta na Dybala # Chelsea wamfuata Cancelo

https://www.sofascore.com/news/wp-content/uploads/2017/08/ousmane-dembele-borussia-dortmund-fc-barcelona-tra.jpg



DORTMUND- BARCELONA wamewasilisha mezani ofa yenye thamani ya pauni milioni 90 (sh bilioni 261), kwa Borussia Dortmund ili kumsajili kinda wa Ufaransa, Ousmane Dembele (20) anayekipiga Signal Iduna Park. Hata hivyo dau hilo limekataliwa. Sky Sports.

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/658/633/hi-res-4b36fafa14a3ae9b5cc73570c7eb39ad_crop_north.jpg?h=533&w=800&q=70&crop_x=center&crop_y=top
PSG wanakaribia kumsaini kinda hatari wa Monaco, Kylian Mbappe (18) kwa dau linalodaiwa kuwa pauni milioni 180 (sh bilioni 522). Mchezaji huyo amekuwa akiwindwa na Real Madrid, Manchester City na Arsenal. Gazzetta dello Sport.

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2016/0106/r41868_1296x729_16-9.jpg&w=738&site=espnfc
Real Madrid inadaiwa kukutana kwa siri na kufanya mazungumzo na windo la Barcelona, Paulo Dybala (23) kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo wa Juventus na Argentina. Don Balon.

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/647/497/hi-res-f0c858a6ff39d55e4de3cd971be05bd0_crop_north.jpg?h=533&w=800&q=70&crop_x=center&crop_y=top
Chelsea wameendelea kutumaini kuwa Valencia watawakubalia ofa yao ya kumsajili beki wao, Joao Cancelo (23). Sky Sports.

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2017/0118/r172206_1296x729_16-9.jpg&w=738&site=espnfc
Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho ameliweka jina la Danny Rose (27) nafasi ya kwanza katika orodha ya majina ya wachezaji anaowahitaji kwa ajili ya msimu ujao. Daily Record.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/06/nintchdbpict000327490350-e1496845573248.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Arsene Wenger amesema klabu yake ya Arsenal haina matumaini makubwa ya kumshawishi staa wa timu hiyo, Alexis Sanchez (28) kubaki Emirates. Pia timu hiyo imempa ofa ya mshahara wa pauni 300,000 (sh milioni 870) kwa wiki. Daily Mail.

http://i4.mirror.co.uk/incoming/article10961713.ece/ALTERNATES/s615/Liverpool-FC-Training-Session-in-Germany.jpg
Mchambuzi wa soka la Hispania, Graham Hunter amesema Barcelona hawataweza tena kumsajili kiungo wa Liverpool, Philippe Coutinho (25), iwapo watafanikiwa kumsainisha winga wa Borussia Dortmund, Ousmane Dembele (20). BBC Radio 5.

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/02/06/25656DDA00000578-2942774-image-a-7_1423235101745.jpg
Mwenyekiti wa Tottenham Hotspurs, Daniel Levy yuko katika mtanziko mkubwa kuhusu mishahara kiduchu wanayolipwa wachezaji wa timu hiyo. Wengi wametishia kuondoka wakiongozwa na Danny Rose (27) ambaye Levy amesema atamuuza kwa pauni milioni 50 (sh bilioni 145). Daily Mail.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/08/nintchdbpict000342650518.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Arsenal wana matumaini ya kumbakiza klabuni hapo kiungo wao, Mesut Ozil (28), baada ya Mjerumani huyo kusema anajiandaa kukubali mshahara wa pauni 225,000 (sh milioni 652.5) kwa wiki. The Sun.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/05/nintchdbpict000321021590.jpg?strip=all&w=960&quality=100
PSG wanajiandaa kumtoa mshambuliaji wao Javier Pastore (28) na fedha, kwa ajili ya kumsajili kipa wa Atletico Madrid na Slovenia, Jan Oblak (24). AS.

http://i2.mirror.co.uk/incoming/article9751445.ece/ALTERNATES/s1200/William-Carvalho.jpg
West Ham wameweka mezani mwa Sporting Lisbon dau la pauni milioni 30 (sh bilioni 87), kwa ajili ya kupata huduma ya kiungo wa timu hiyo ya Ureno, William Carvalho (25). Telegraph.

No comments

Powered by Blogger.