Header Ads

Trump aichimba mkwara Korea Kaskazini



https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/7ED4/production/_97286423_trump.jpg

WASHINGTON DC- RAIS Donald Trump ameitahadharisha Korea Kaskazini kwamba, inafaa kuwa na ‘wasiwasi sana’ iwapo itatenda lolote kwa Marekani.
Amesema utawala wa taifa hilo utakuwa shida kubwa ‘ambayo ni mataifa machache yaliyowahi kukumbana nayo’ iwapo ‘hawatabadilika’.
Amesema hayo saa chache baada ya Korea Kaskazini kutangaza kwamba, ina mpango wa kurusha makombora manne karibu na kisiwa cha Marekani cha Guam.
Akiongea Alhamisi Bedminster, New Jersey, Trump alidokeza kuwa huenda taarifa zake kuhusu Korea Kaskazini hazijakuwa na ukali wa kutosha, licha ya kuionya Korea Kaskazini wiki hii kwamba itanyeshewa na ‘moto na ghadhabu’ kutoka kwa Marekani.
Trump alishutumu Serikali za awali za Marekani, akisema zilionesha udhaifu kukabiliana na Korea Kaskazini na pia akashutumu mshirika wa karibu wa Korea Kaskazini, akisema kwamba inafaa ‘kufanya juhudi zaidi’.
Alisema: “Nawaambia, iwapo Korea Kaskazini itafanya jambo lolote hata kwa kufikiria tu kuhusu kumshambulia mtu tunayempenda au tunayemuwakilisha au mshirika wetu au sisi wenyewe inaweza kuwa na wasiwasi sana, sana.”
Waziri wa Ulinzi nchini, James Mattis ametahadharisha kwamba, mzozo wa kivita na Korea Kaskazini utakuwa na ‘madhara makubwa’ na akadokeza kwamba juhudi za kidiplomasia kwa sasa zinaanza kuzaa matunda.
“Juhudi za Marekani zinaongozwa na diplomasia, zina msukumo wa kidiplomasia, na zinapata matokeo kidiplomasia,” alisema Mattis.
Hata hivyo, Korea Kaskazini imepuuzilia mbali vitisho vya Marekani na kuziita ni ‘upuuzi’.
BBC

No comments

Powered by Blogger.