Header Ads

Tetesi Asubuhi; Barcelona waigwaya Liverpool # Chelsea wakataliwa Sandro # Man United wamuota Perisic



https://metrouk2.files.wordpress.com/2017/05/686314800.jpg

LONDON- MKURUGENZI wa Michezo wa Barcelona, Robert Fernandez amesema itakuwa vigumu kumsajili kiungo wa Liverpool, Philippe Coutinho (25), kwa kuwa hana kipengele cha kumruhusu kuondoka. Hata hivyo, wamesema watapambana hadi dirisha la usajili litakapofungwa. Liverpool Echo.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict0003351126033.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Kwa mara nyingine tena, Chelsea imeendelea kugonga mwamba kwenye mpango wao wa kumsajili beki wa Juventus na Brazil, Alex Sandro (26), baada ya ofa yao ya pauni milioni 63 (sh bilioni 182.7) kukataliwa. Mirror.

http://e0.365dm.com/17/05/16-9/20/skysports-ivan-perisic-inter-milan_3964812.jpg?20170528120928
Manchester United bado hawajakata tamaa kuhusiana na mpango wao wa kumsajili winga wa Inter Milan, Ivan Perisic (28), licha ya United kutoa pauni milioni 39 (sh bilioni 113.1). Mirror.

https://img.rasset.ie/000d59bc-800.jpg
Manchester City wako tayari kutoa pauni milioni 22 (sh bilioni 63.8), kwa ajili ya kumsajili beki wa West Brom, Jonny Evans (29), baada ya dau lao la kwanza kukataliwa. Evans anatarajiwa kulipwa pauni 75,000 (sh milioni 217.5) kwa wiki Etihad. Mirror.

http://www.markingthespot.com/wp-content/uploads/2017/08/dembele-bvb.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Borussia Dortmund amesema Barcelona hawako karibu kukamilisha usajili wa winga wao, Ousmane Dembele, kwani hawajafikia matakwa ya klabu hiyo ya Signal Iduna Park. Kicker.

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/05/27/11/40CFB4B300000578-4547440-image-m-4_1495879900902.jpg
Tottenham wako karibu kuinasa saini ya beki wa kati wa Ajax na Colombia, Davinson Sanchez (21), kwa ada ya pauni milioni 28 (sh bilioni 81.2) na ongezeko la pauni milioni 14 (sh bilioni 40.6). Independent.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict0003274565322.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Mshambuliaji mahiri wa Chelsea, Diego Costa (28) amesema hatarudi Stamford Bridge kamwe na anajiandaa kujiunga na Atletico Madrid. Mchezaji huyo kwa sasa yuko kwao Brazil. Telegraph.

https://s-media-cache-ak0.pinimg.com/originals/f5/1a/a1/f51aa127689c02613de06e702f70dbe6.jpg
Beki wa Arsenal na Brazil, Gabriel (26) yuko karibu kukamilisha uhamisho wa kwenda Valencia, kwa ada yenye thamani ya pauni milioni 10 (sh bilioni 29). Evening Standard.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict0003274565322.jpg?strip=all&w=960&quality=100  
Everton inapanga kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa (28) ambaye kocha wa Chelsea, Antonio Conte alimwambia hayupo kwenye mipango yake. Sun.

http://cdn.images.dailystar.co.uk/dynamic/122/photos/413000/900x738/840413.jpg
PSG wanasema bado wana mpango wa kumsajili kiungo wa Monaco na Brazil, Fabinho (23). L’Equipe.

http://www.footmercato.net/images/a/matuidi-n-est-toujours-pas-un-joueur-de-la-juventus_208333.jpg
Kiungo wa PSG, Blaise Matuidi (30) amekamilisha uhamisho wake wa kwenda Juventus lakini bado klabu hizo hazijakubaliana kuhusu ada. Kocha wa PSG, Unai Emery hataki kumuuza mchezaji huyo. Le Parisien.

http://cdn3-i.hitc-s.com/389/croatias_nikola_kalinic_celebrates_scoring_their_first_goal_275152.jpg
Uongozi wa Fiorentina umemwambia mshambuliaji wao raia wa Croatia, Nikola Kalinic (29), atapigwa faini kutokana na kutoripoti mazoezini jana. Kalinic anawindwa na AC Milan. Sun.

No comments

Powered by Blogger.