Harry Kane, Sanchez, Kante na Hazard kuwania Ballon d’Or
Mshambuliaji
huyo wa Tottenham, atajiunga na Alexi Sanchez, viungo wa kati wa Chelsea, Eden
Hazard na N'Golo Kante katika orodha ya wachezaji 24.
Mshindi
wa mwaka uliopita, Cristiano Ronaldo ameteuliwa pamoja na Lionel Messi wa
Bareclona na nyota wa PSG, Neymar. Zlatan Ibrahimovic ambaye mara ya mwisho
aliichezea Manchester United, pia ameorodheshwa.
Washindi
wataamuliwa na jopo la wakufunzi wa vilabu na wawakilishi wa vyombo vya habari
na mashabiki.
Upigaji
kura unakamilika Septemba 7 na washindi watatangazwa katika sherehe ya kutoa
zawadi Okotoba 23.
BBC
No comments