Kim Jong-un akabidhiwa mpango wa kukishambulia kisiwa cha Marekani

PYONGYANG- VYOMBO vya habari nchini, vimeripoti kuwa Kiongozi
wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un amekabidhiwa rasmi ripoti ya taifa yenye mpango
wa kutaka kurusha kombora hadi katika kisiwa cha Guam kilichopo eneo la pacific
na kinachomilikiwa na Marekani.
Hata hivyo,
ripoti hiyo imesema kuwa itachunguza vitendo vya Marekani kabla ya kuchukua
hatua ya kurusha kombora hilo katika kisiwa hicho.
Wiki iliyopita,
Korea Kaskazini ilionya kwamba mikakati inawekwa kushambulia eneo hilo ambalo
ndegevita za Marekani zimeweka kambi na kuongeza urushianaji maneno baina ya
mataifa hayo mawili hasimu.
Ripoti hiyo
ya kitengo cha habari cha KCNA, ilisema Kim aliutazama mpango huo kwa muda
mrefu na kuujadili na maofisa wakuu wa jeshi. Kamanda wa jeshi la kimkakati la
Korea Kaskazini, sasa anasubiri agizo baada ya kuandaa shambulio hilo la Guam.
Ripoti hiyo imeongezea
kwamba, Kim atachunguza mienendo ya Marekani kabla ya kutoa uamuzi wowote,
hatua inayoonekana kupunguza kasi ya cheche za maeneo kati ya mataifa hayo mawili.
Mwandishi wa
BBC, Yogita Limaye aliyepo mjini Seoul, anasema hatua hiyo itapunguza wasiwasi
na kuzuia mgogoro wa kijeshi katika eneo la Korea.
Mwandishi mwingine
ameongeza kuwa, baada ya siku kadhaa za vitisho kutoka Pyongyang, inaonekana
kwamba Rais Kim sasa anataka kunyamaza na kutazama hali, lakini katika taifa
lenye siri kubwa kama Korea Kaskazini huwezi kuwa na hakika.
Wachanganuzi
wanasema, hali hiyo inamaanisha kwamba Pyongyang haiko tayari kutekeleza
shambulio katika kisiwa cha Guam, hivyo huenda inachukua muda.
Hatua hiyo
inajiri baada ya Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis kuonya kwamba
shambulio lolote linaweza kusababisha vita vikali, na iwapo Pyongyang itarusha
kombora kuelekea Guam basi ‘itakuwa vita’.
Amewaambia waandishi
wa habari kwamba, Jeshi la Marekani litatetea taifa hilo iwapo kutakuwa na
shambulio lolote wakati wowote na kutoka kwa taifa lolote.
Pia, aliwahakikisha raia wa Guam, ambapo kuna kambi za kijeshi za
Marekani kwamba, takriban watu 160,000 wanalindwa na akasema iwapo kombora
litarushwa ‘tutalitibua’.
BBC
No comments