Header Ads

Nahodha wa Mexico awekewa vikwazo Marekani



http://www.tabascohoy.com/imagenes/2017/04/13/rafa2.jpg

MEXICO CITY- SERIKALI ya Marekani imemuorodhesha mchezaji wa mpira wa miguu na nahodha wa timu ya taifa ya Mexico, Rafael Marquez (38) kama mmoja wa watu 22 waliowekewa vikwazo na taifa hilo kutokana na dawa za kulevya.
Mamlaka za Marekani, zimeeleza kuwa Marquez amekuwa ni mmoja kati ya watu wenye mahusiano ya karibu na mmoja wa mfanyabiashara wa dawa hizo nchini, Raul Flores Hernandez pamoja na magenge ya Sinaloa, na Jalisco New Generation Gang yanayojihusisha na dawa hizo.
“Raul Flores Hernandez amekuwa akifanya kazi hiyo ya dawa za kulevya kwa miongo mingi, kutokana na mahusiano yake na watu na magenge mengine. Anawatumia marafiki zake kuficha biashara zake,” ilisema taarifa ya John E. Smith ambaye ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mali za Nje katika ofisi ya Hazina ya Marekani.
DW

No comments

Powered by Blogger.