Header Ads

Mawakala wapitia fomu za matokeo usiku kucha Kenya

https://ichef.bbci.co.uk/live-experience/cps/624/cpsprodpb/vivo/live/images/2017/8/10/8bdbdba2-e206-47dc-97c7-78eff6ef735b.jpg

Ajenti wa Raila
Ajenti wa RailaAjenti wa RailaAjenti wa RailaAjenti wa Raila

NAIROBI- WAKATI matokeo rasmi yakisubiriwa kwa hamu zaidi, usiku wa kuamkia leo ulikuwa ni usiku uliotawaliwa na shughuli nyingi hususan katika kituo cha taifa cha kujumlishia matokeo ya uchaguzi maarufu Bomas.
Maajenti wa vyama vya siasa, walikuwa wakikagua Fomu 34A za matokeo kutoka vituo vya kupigia kura katika sehemu maalum.
Mgombea wa upinzani, Raila Odinga alikuwa amelalamika awali kwamba IEBC ilikuwa ikitangaza matokeo bila kutoa fomu hizo. Tume hiyo baadaye ilitoa fomu hizo. 
Matokeo BomasMatokeo Bomashttps://ichef.bbci.co.uk/live-experience/cps/624/cpsprodpb/vivo/live/images/2017/8/10/91ac2fde-2ff5-4840-a7bc-d93a24979b02.jpg
Kufikia sasa ni vituo 1,200 pekee kati ya 40,883 ambavyo havijawasilisha matokeo. Tume ya uchaguzi imeahidi kutoa maelezo kuhusu matokeo yaliyo kwenye fomu zilizopokelewa Bomas baadaye leo.
Kwa upande mwingine, IEBC imekanusha vikali madai yote yaliyotolewa na Raila jana kwamba mtandao wa tume hiyo uliingiliwa (kudukuliwa) na wadukuzi na kubadilisha matokeo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.