Header Ads

Asubuhi Yetu; Mourinho awataka Rose na Perisic # PSG wamkomalia Mbappe # Barcelona wamng’ang’ania Coutinho



https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/02/nintchdbpict000299064198-e1487457525308.jpg?strip=all&w=960

MANCHESTER- KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho amesema ameshauambia uongozi wa klabu hiyo ufanye haraka usajili wa beki wa pembeni wa Tottenham Hotspurs, Danny Rose (27) na winga wa Inter Milan, Ivan Perisic (28). Manchester Evening News.

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/03/12/02/3E2B5C4700000578-4304990-Kylian_Mbappe_scored_his_Monaco_s_second_as_they_downed_Bordeaux-a-126_1489284110144.jpg
Paris St-Germain (PSG) wako katika hatua za mwisho za kumsajili mshambuliaji kinda wa Monaco, Kylian Mbappe (18) kwa dau la pauni milioni 163 (sh bilioni 472.7). PSG pia imeweka mezani ofa nzuri kwa Monaco, kwa ajili ya kiungo wao, Fabinho (23). Daily Record.

http://e2.365dm.com/16/09/16-9/20/premier-league-football-liverpool-free-kick-philippe-coutinho_3793367.jpg?20160924173130
Barcelona wanatarajiwa kurudi kwa mara ya nne mezani mwa Liverpool, baada ya dau lao la tatu la pauni milioni 90 (sh bilioni 261) kwa ajili ya kumsajili Philippe Coutinho (25) kukataliwa Anfield. Daily Mail.

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2016/01/11/22/2FE041FE00000578-0-image-a-1_1452550197984.jpg
Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika kutoka Ufaransa, endapo Kylian Mbappe (18) ataondoka Monaco, basi klabu hiyo italazimika kumsajili mshambuliaji wa AC Milan, Carlos Bacca (30). Sun.

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2016/01/13/05/2FF59E0C00000578-3396902-image-a-22_1452663871311.jpg
Chelsea imetoa pauni milioni 35 (sh bilioni 101.5) kwa Arsenal, kama ada ya kumsajili winga wa timu hiyo Alex Oxlade-Chamberlain (23) aliyebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake klabuni hapo. Daily Star.

http://cdn1.dailypost.ng/wp-content/uploads/2016/12/Alexis-Sanchez-.jpg
Arsenal wameeleza kuwa wanahofia mshambuliaji wao raia wa Chile, Alexis Sanchez (28) huenda akaanzisha tena harakati zake za kutaka kuondoka klabuni hapo. Daily Mirror.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiRIcQopSmPNcv0H3lP0B78DxE_RLhFn_hzogX6WDUoaF_IUve4v0mGT8abVQiYfvrJcspWxSTQm_TklOW5eBcBv2SpxePOEEkK95wCkfyo6C5NxFIl-GY1IdHfAcNAc7NRFPoQv_Q1jAw/s1600/willian.jpg
Inadaiwa kuwa winga wa Chelsea na Brazil, Wilian (29) amefanya mazungumzo na Manchester United, kwa ajili ya kujiunga tena na kocha wake wa zamani, Jose Mourinho ambaye awali walifanya kazi wote Stamford Bridge. Goal.

https://static.standard.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2016/11/22/10/dannyrose2211.jpg
Beki wa pembeni wa Tottenham anayewindwa na Manchester United, Danny Rose (27) ameitaka klabu yake kutumia fedha kusajili wachezaji lakini si wale ambao itakupasa uanze kutumia mtandao wa Google kutafuta huyo ni nani. The Sun.

https://images2.footballwhispers.com/wp-content/uploads/2017/04/25150446/William-Carvalho-Sporting-West-Brom.jpg
West Ham wanapanga kutoa pauni milioni 25 (sh bilioni 72.5) kwa Sporting Lisbon ya Ureno, kama ada ya uhamisho wa kiungo mahiri wa timu hiyo, William Carvalho (25). Daily Mail.


No comments

Powered by Blogger.