Header Ads

Korea Kaskazini: Tutakishambulia kisiwa cha Marekani siku chache zijazo



Map showing Guam

PYONGYANG- SERIKALI inasema mpango wake ya kufyatua makombora kwenda kisiwa cha Marekani cha Guam, utakuwa tayari hivi karibuni huku majibizano ya kivita na Marekani yakiendelea.
Vyombo vya habari nchini, vilieleza kuwa makombora ya Hwasong-12 yatapita anga ya Japan na kuanguka baharini karibu kilomita 30 kutoka kisiwa cha Guam ikiwa mpango huo utaidhinishwa na Rais Kim Jong-un. 
https://pbs.twimg.com/media/C_1DDqPUIAALpxJ.jpg
Serikali imepuuza onyo la Rais wa Marekani, Donald Trump kuwa itashambuliwa vikali. Marekani imeionya Korea Kaskazini ikisema kuwa, vitendo vyake vinamaanisha kuwa huo utakuwa mwisho wa utawala wa nchi hiyo.
Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Jim Mattis alisema Korea Kaskazini itashindwa vibaya ikiwa itaingia vitani na Marekani na washirika wake.
Korea Kaskazini ilitangaza jana kuwa inachora mipango ya kufanya mashambulizi ya makombora katika kisiwa hicho kilicho na kambi za jeshi la Marekani na watu 163,000
Taarifa iliyotolewa baadaye, ilisema jeshi litakamilisha mpango huo ifikapo kati kati mwa mwezi huu na kupeleka kwa kiongozi wao Kim Jong-un kuidhinishwa.
BBC

No comments

Powered by Blogger.