Header Ads

Maporomoko ya ardhi yaua 40 DRC



https://ichef.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/102D5/production/_97416266_ituri_drcongo_swahili.png

KINSHASA- WATU zaidi ya watu 40, wameuawa kwenye janga la maporomoko ya ardhi ambalo limetokea Kaskazini Mashariki mwa nchi katika eneo la karibu na Ziwa Albert.
Wengi wa wale waliopoteza maisha katika tukio hilo, ni watu wa kijiji kimoja kinachofanya uvuvi katika kingo za Ziwa Albert.
Mvua kubwa imesababisha sehemu za mlima ulio karibu kuporomoka na kufunika kijiji hicho kwa mujibu wa shirika la habari la AFP. Watu wengine kadhaa, walifariki wakitafuta dhahabu kwenye migodi ya zamani.
Kumekuwa na majanga mabaya ya maporomoko ya ardhi, katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo miaka ya hivi karibuni.
Janga hilo linatokea baada ya mafuriko mabaya yaliyotekea kwenye mji wa Freetown nchini Sierra Leone, siku ya Jumatatu ambapo zaidi ya watu 300 waliuawa.
Ripoti zinasema kuwa watu 28 walizikwa jana huku 12 wengine walizikwa leo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.