Polisi watibua shambulio la pili Barcelona
Kwa
mujibu wa taarifa za awali zilizotolewa na Polisi, washambuliaji walikuwa
wamevalia vilipuzi.
Watu
13 walifariki huku makumi wakijeruhiwa, baada ya gari dogo kuingia katika eneo
la watu mjini Barcelona eneo la Las Ramblas jana mchana.
Dereva
wa gari hilo alitoroka na bado anaswaka. Waziri Mkuu, Mariano Rajoy alisema
kuwa lilikuwa shambulio la kijihadi.
Mamlaka
sasa zinahusisha shambulio hilo la Barcelona pamoja na lile la Camrils, huku
mlipuko ukiripotiwa katika nyumba moja juzi Jumatano jioni katika mji wa
Alcanar ambapo mtu mmoja alifariki.
Awali,
Ofisa Mkuu wa Polisi, Josep Lluis Trapero alisema kuwa inaonekana wakazi wa eneo
la Alcanar walikuwa wakiandaa kutengeneza kilipuzi.
Mjini
Cambrils, watu saba akiwemo ofisa mmoja wa polisi walijeruhiwa wakati gari
lilipovurumishwa katika umati wa watu mapema leo kulingana na huduma za dharura
huko Catalan.
Mtu
mmoja yuko katika hali ya mahututi.
Vyombo
vya habari nchini, vimeripoti kwamba washambuliaji waliuawa wakati walipojaribu
kutoroka baada ya gari lao kupinduka. Baadaye misururu ya milipuko ilifuatia.
BBC
No comments