Liverpool waidunda Hoffenheim na kunusa makundi UEFA
BERLIN- MABINGWA mara tano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Liverpool, wamejiweka
katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya makundi baada ya kuitandika Hoffenheim
bao 2-1.
Mchezo huo
ambao ulikuwa mkali zaidi, ulishuhudia beki kinda wa Liverpool, Trent
Alexander-Arnold akiiweka mbele timu yake na kisha bao la pili likawekwa
kimiani na Havard Nordtveit ambaye alijifunga kutokana na mpira wa krosi
uliopigwa na James Milner.
Bao la
Hoffenheim liliwekwa kimiani na Mark Uth.
No comments