Header Ads

Kombora la kivita lililoibwa lalipuka kiwandani Urusi



https://ichef-1.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/15D0F/production/_97295398_93436256.jpg

CHITA- Kombora la kutungua ndege ambalo lilikuwa limebiwa na watu wasiojulikana, limelipuka na kuwaua watu wawili na kumjeruhi mmoja nchini.
Kombora hilo la urefu wa mita 10 (futi 35) ambalo liliundwa wakati wa enzi za Sovieti, lililipuka likiwa katika kiwanda cha kutengeneza bidhaa mpya kutoka kwa bidhaa chakavu Mashariki mwa nchi.
Vyombo vya habari nchini, vilifahamishwa kuhusu mlipuko wa kombora hilo kubwa mjini hapa, baada ya video ya mlipuko huo iliyokuwa imepigwa na mtu mmoja akitumia kamera ya gari kuiweka YouTube.
Kombora hilo ni la aina ya S-200 Angara, ambayo hufahamika kama SA-5 ‘Gammon’ katika mataifa ya Nato.
Makombora hayo yamekuwa yakitumiwa tangu miaka ya 1960, lakini siku hizi nafasi yake imeanza kuchukuliwa na makombora aina ya S-300 na S-400. Haijabainika ni vipi kombora hilo lilifika katika kiwanda hicho.
Tovuti ya by24.org, inasema kwamba kombora hilo la uzani wa tani saba liliibiwa kutoka kwenye kambi ya jeshi na watu wasiojulikana na kuuziwa wakuu wa kiwanda hicho.
Lililipuka wakati wafanyakazi walipokuwa wakijaribu kulibomoa. Tovuti ya The Insider, ilisema wafanyakazi wa dharura walipata kombora jingine aina ya S-200 ambalo halikuwa limebomolewa.
Kisa hicho kimezua mjadala mkali katika mitandao ya kijamii, wengi wakishangaa ilikuwaje hadi kombora likawa katika kiwanda hicho.
“Tuna silaha nyingi chakavu nchini, kiasi kwamba watu wanaziuza kama vyuma vikukuu,” aliandika mmoja wa watu kwenye mtandao wa VKontakte. Alisema hilo linaweza kusababisha madhara makubwa.
BBC

No comments

Powered by Blogger.