Kivumbi cha EPL chashuhudia nyavu zikitikishwa mara 31

LONDON- PAZIA la Ligi Kuu nchini (EPL), limefunguliwa rasmi Ijumaa
ilyopita kwa mechi kali baina ya Arsenal na Leicester City na michezo mingine
ambayo ilishuhudia nyavu zikitikiswa mara 31.
Mchezo huo ambao ulikuwa wa kwanza na uliokuwa ukisubiriwa na mashabiki
wengi, ulishuhudia jumla ya mabao 7 yakitinga nyavuni mwa timu zote mbili.
Arsenal ndiyo waliokuwa wa kwanza kuandika bao lao kupitia kwa
mshambuliaji wao mpya Alexandre Lacazette, mnamo dakika ya kwanza kabla ya
kusawazishwa na Jamie Vardy.
Mara baada ya mabayo hayo, mchezo huo ulishuhudia bao tano nyingine
zikitingisha nyavu. Arsenal wailazimika kusawazisha na kisha kuibuka na ushindi
wa bao 4-3.
Michezo mingine ambayo ilifuata Jumamosi, ilikuwa ni baina ya Liverpool
na Watford, mchezo ambao ulihusisha mabao sita baada ya kuisha kwa sare ya bao
3-3.
Chelsea ambao mabingwa hao watetezi waliangukia pua kwa kufungwa bao 3-2
na Burnley, huku wababe hao wa Stamford Bridge wakiwapoteza Garry Cahill na
Cesc Fabregas ambao walioneshwa kadi nyekundu kila mmoja. Crystal Palace
waliduwazwa na wageni Huddersfield Town kwa kuchapwa bao 3-0.
Bao pekee la Wayne Rooney, liliiwezesha klabu yake ya utotoni ikiibuka na
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Stoke City. Ingizo jipya la West Bromwich Albion,
Ahmed Hegazy, liliing’arisha timu hiyo kwa kufunga bao lililoipa ushindi wa 1-0
dhidi ya AFC Bournemouth.
Mchezo wa jioni baina ya Manchester City dhidi ya wageni wa ligi,
Brighton Hove and Albion, ulishuhudia City ikiibuka na ushindi wa bao 2-0 kwa
magoli ya Sergio Aguero na Lewis Dunk aliyejifunga.
Jana Jumapili, EPL iliendelea kwa michezo miwili baina ya Newcastle
United vs Tottenham Hotspurs na Manchester United na West Ham United.
Spurs iliibuka na ushindi wa bao 2-0, kupitia Dele Alli na Ben Davies
huku Jonjo Shelvey akioneshwa kadi nyekundu, baada ya kumkanyaga makusudi Dele
mbele ya mwamuzi.
Man United waliibuka na ushindi wa bao 4-0, kupitia kwa Romelu Lukaku
aliyefunga mara mbili kabla ya Paul Pogba na Anthony Martial kufunga goli moja
moja.
Vinara wa magoli hadi kufikia sasa ni;
Jina la
Mchezaji
|
Timu
anayotoka
|
Idadi ya
magoli
|
Jamie Vardy
|
Leicester City
|
2
|
Steve Mounie
|
Huddersfield Town)
|
2
|
Romelu Lukaku
|
Manchester United)
|
2
|
Alexandre Lacazette
|
Arsenal
|
1
|
Shinji Okazaki
|
Leicester City
|
1
|
Aaron Ramsey
|
Arsenal
|
1
|
Danny Welbeck
|
Arsenal
|
1
|
Olivier Giroud
|
Arsenal
|
1
|
Stefano Okaka
|
Watford
|
1
|
Abdoulaye Doucoure
|
Watford
|
1
|
Miguel Britos
|
Watford
|
1
|
Sadio Mane
|
Liverpool
|
1
|
Paul Pogba
|
Manchester United
|
1
|
Anthony Martial
|
Manchester United
|
1
|
Dele Alli
|
Tottenham Hotspurs
|
1
|
Ben Davies
|
Tottenham Hotspurs
|
1
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
No comments