Header Ads

CIA: Hakuna uwezekano wa kutokea vita vya nyuklia na Korea Kaskazini



https://stonecoldtruth.com/wp-content/uploads/2017/04/Untitled-design-29.jpg

WASHINGTON DC- MKURUGENZI wa Shirika la Ujasusi Marekani (CIA), Mike Pompeo ameeleza kuwa hakuna uwezekano wala tishio lolote la kutokea vita vya nyuklia baina ya Marekani na Korea Kaskazini licha ya kuongezeka kwa msukosuko.
Pompeo alisema kuwa, Korea Kaskazini inaendelea kwa kasi na mipango yake ya nyuklia na jaribio lolote la kombora halitakuwa la kutia wasiwasi.
Hata hivyo, Pompeo ameonya kuwa uvumilivu wa Marekani unafikia kikomo. Pande zote mbili zimetupiana maneno makali huku Rais Donald Trump akitishia kuikabili vikali Korea Kaskazini.
Pompeo anasema ana uhakika kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un atajaribu kuendelea na mpango wa nyuklia wa nchi hiyo.
Alipoulizwa kuhusu muda gani Korea Kaskazini wamebaki nao, kabla ya kuunda silaha ya nyuklia ambayo inaweza kushambulia Marekani, alisema kuwa wako karibu.
Msukosuko wa siku nyingi kuhusu mpango wa nyukilia wa Korea Kaskazini, uliongezeka zaidi wakati taifa hilo lilipofanya jaribio la makomboa mawili ya masafa marefu mwezi uliopita.
Hatua hiyo, ilisababisha awamu nyingine ya vikwazo vya kiuchumi vya Umoja wa Mataifa hatua iliyoghadhabisha utawala wa Kim.
Trump alisema kuwa jeshi la la Marekani liko tayari, huku Korea Kaskazini ikimlaumu kwa kuchochea vita katika rasi ya Korea.
BBC

No comments

Powered by Blogger.