Header Ads

Raila kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani



https://ichef-1.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/F2C2/production/_97264126_040999630-1.jpg

NAIROBI- KIONGOZI wa Muungano wa Upinzani na aliyekuwa mgombea wa urais Kenya, Raila Odinga amesema atakwenda Mahakama ya Katiba kwa ajili ya kupinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Agosti 8, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari na wananchi waliojitokeza kumsikiliza, Raila alisema maamuzi hayo yamefikiwa kutokana na NASA kutoridhishwa na mwenendo mzima wa uchaguzi huo na kuongeza kuwa matokeo yalichakachuliwa.
Aidha, Raila alisema Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC) ilitangaza matokeo hayo huku kukiwa na upungufu wa baadhi ya fomu za kujumlishia matokeo maarufu kama 34A na 34B.
“Kama NASA, hatujaridhishwa na namna mchakato wa kuhesabu na kutangaza matokeo uluvyokuwa. Hivyo tunakwenda Mahakama ya Katiba kupinga matokeo yaliyotengenezwa kwa kompyuta, ili kumpa ushindi Uhuru Kenyatta na mwenzake William Ruto,”
“Wakenya wanahuzunika kwani walijitokeza kwa wingi, ili kuchagua kiongozi wanayempenda lakini sauti yao imemezwa na kompyuta iliyotumika kuzalisha matokeo hayo na kuipa ushindi Jubilee,” alisema Raila.

No comments

Powered by Blogger.