Header Ads

Ronaldo ashushiwa rungu kali Hispania



http://cdn-01.independent.ie/incoming/article36028791.ece/6fd64/AUTOCROP/w620h342/Ronaldo%20.jpg

MADRID- MSHAMBULIAJI mahiri wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo (32) amefungiwa kucheza mechi tano baada ya kumsukuma mwamuzi aliyemuonesha kadi nyekundu kwenye mchezo dhidi ya mahasimu wao wakubwa Barcelona jana.
Mreno huyo ambaye aliingia akitokea benchi, aliifungia timu yake bao la pili ambalo lilisababisha apewe kadi ya njano kwa kuvua jezi. Kadi ya pili ya njano na nyekundu, zilikuja baada ya mchezaji huyo kudaiwa kujiangusha kwa ajili ya kutafuta penati.
Mara baada ya kujiangusha, mwamuzi wa mchezo huo alimuonesha Ronaldo kadi ya pili ya njano kisha nyekundu ambayo ilisababisha mchezaji huyo kumsukuma mwamuzi huyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya shirikisho la soka Hispania, Ronaldo anakosa mchezo mmoja kutokana na kadi hizo na mingine minne ikiwa ni adhabu ya kitendo cha utovu wa nidhamu cha kumsukuma mwamuzi.
Ronaldo atakosa mchezo wa marudiano dhidi ya Barcelona kwenye kombe hilo la Super Cup, unaotarajiwa kuchezwa Jumatano jijini hapa. Pia mchezaji huyo atakosa michezo mingine minne ya La Liga dhidi ya Deportivo La Coruna, Valencia, Levante na Real Sociedad.
Hata hivyo, Real Madrid wamepewa siku 10 za kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo.
Independent.

No comments

Powered by Blogger.