China yafungua kambi ya kijeshi Djibouti
Kambi
hiyo, itatumika kusambaza meli za wanamaji wake wanaoshiriki shughuli za kulinda
amani na mipango ya kibinadamu katika pwani ya Yemen na hususan Somalia.
Ni
kambi ya kwanza ya wanamaji katika taifa la kigeni, ijapokuwa maofisa wa China
wameitaja kuwa eneo la kupanga mikakati. Kambi hiyo itasaidia China kuimarisha
doria zake katika maji yasiyo ya Somalia na Yemen, mbali na kutekeleza majukumu
yake ya kibinadamu.
Licha
ya Djibout kuwa na eneo dogo, ina kambi za kijeshi za Marekani na Ufaransa.
No comments