Header Ads

Waziri Mkuu Pakistan ajiuzulu



http://bsmedia.business-standard.com/_media/bs/img/article/2016-09/20/full/1474355608-3453.jpg

ISLAMABAD- WAZIRI Mkuu wa Pakistan, Nawaz Sharif amejiuzulu wadhifa huo baada ya Mahakama Kuu nchini kumzuia kushika wadhifa wowote Serikalini kufuatia uchunguzi kwa madai ya ufisadi.
Uamuzi huo, unakuja baada ya uchunguzi kuhusu utajiri wa familia yake na ufichuzi wa mwaka 2015 wa Panama Papers, uliowahusisha watoto wake na akaunti za benki ugenini.
Sharif mara kwa mara amekuwa akikana kufanya lolote baya.
Amri hiyo ilitolewa na jopo la majaji watano. Mahakama ilifurika leo na usalama zaidi uliimarishwa katika viunga vyote vya mahakama hiyo na mji huu huku maelfu ya wanajeshi na polisi wakimwagwa mitaani.
Waziri wa Mambo ya Ndani nchini nchini, Chaudhry Nisar Ali Khan, alimshauri Sharif kukubali uamuzi wa leo.
Mahakama imependekeza kufunguliwa kwa kesi za ufisadi, dhidi ya watu kadhaa akiwemo Sharif, mtoto wake wa kike, Maryam na mumewe Safdar, Waziri wa Fedha, Ishaq Dar na wengine kadhaa.
Hakuna Waziri Mkuu wa Pakistan aliye raia ambaye alishawahi kumaliza kipindi chake cha miaka mitano cha uongozi.

No comments

Powered by Blogger.