Header Ads

Aliyeua wazazi na majirani 17 ahukumiwa kifo China



http://wickes.scene7.com/is/image/travisperkins/largeNormal/Demolition-Tools-Wickes-Professional-Contractor-Pick-Axe-Head-Handle~T3274_501004_00?defaultImage=travisperkins/missing-product

YUNNAN- MWANAUME mmoja ambaye aliwaua wazazi wake, kisha kuwaua majirani 17 ili kuficha siri amehukumiwa kifo na mahakama ya jimbo.
Yang Quingpei ambaye aliwaua wazazi wake wote wawili, baada ya wazazi kukataa kumkopesha fedha za kwenda kulipa madeni aliyokuwa nayo.
Mara baada ya kutekeleza mauaji hayo ya wazazi wake, inadaiwa kuwa Yang alipata wasiwasi kuwa huenda majirani wamemuona na ndipo alipoua watu wa familia sita za jirani wakiwemo watoto watatu kwa kutumia sururu ndogo.
Inadaiwa kuwa Yang alitoroka, lakini alikamatwa katika mji wa Kunming siku moja baada ya tukio.  Kwa mujibu wa Shirika la Habari la China, katika hukumu yake mahakama ya jimbo ilieleza tukio hilo kuwa la kinyama, kikatili na la kutisha.
“Japokuwa amekiri mwenyewe kutekeleza ukatili huo, na kuelezea masikitiko yake baada ya kuletwa mbele ya sheria, hayo hayatoshi kusababisha ahurumiwe kwenye hukumu yake,” ilisema sehemu ya hukumu.
Sky News

No comments

Powered by Blogger.