Header Ads

Waziri adaiwa kutumia bilioni 1.6/- kununua maua na zawadi Afrika Kusini



https://image.iol.co.za/image/1/process/620x349?source=https://inm-baobab-prod-eu-west-1.s3.amazonaws.com/public/inm/media/file/1/1855514/1431063258/image/3685875836.jpg

DURBAN- CHAMA kikuu cha upinzani cha Democratic Alliance (DA), kimesema kitaomba maelezo ya kina kuhusiana na mayumizi ya fedha zenye thamani ya dola za Marekani 770,000 (sh bilioni 1.6).
Fedha hizo zinadaiwa kutumiwa visivyo mwaka wa fedha 2013/14 na Wizara ya Nyumba na Makazi iliyo chini ya Waziri Lindiwe Sisulu, ambaye ni mtoto wa mpigania uhuru wa Afrika Kusini, Walter Sisulu.
Inadaiwa kuwa, fedha hizo ambazo zinaweza kujenga nyumba 100 za bei nafuu, zilitumika kununua maua na zawadi mbalimbali kwa watumishi wa idara hiyo.
Kubainika kwa matumizi ya fedha hizo, kumekuja hivi karibuni wakati waziri huyo akijibu moja ya maswali yaliyoelekezwa kwake bungeni na kuzua mjadala mkubwa.
DA wanadai kwamba, waziri huyo ambaye kwa sasa anapigania kuchaguliwa kuwania kupitishwa na chama cha ANC kwa ajili ya kugombea urais, anapaswa kuwajibishwa ili ataje wale wote walionufaika na mgawo wa fedha hizo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.