Header Ads

Nyani akata umeme Zambia



A baboon watches tourists along the side of the road July 3, 2010 in Capetown, South Africa
A baboon watches tourists along the side of the road July 3, 2010 in Capetown, South Africahttp://d3n1j8rr5smgk8.cloudfront.net/wp-content/uploads/olive_baboon.jpg

LUSAKA- SHIRIKA la Umeme Zambia (ZESCO), limeeleza kuwa tatizo la umeme kukatika jana katika mji wa Livingstone lilitokana na hitilafu iliyosababishwa na mnyama aina ya nyani.
Msemaji wa Zesco, Henry Kapata, alieleza kuwa nyani huyo aliingia kwenye eneo lenye mitambo mikubwa ya kupoza na kusambaza umeme na kisha kupigwa shoti iliyosababisha kukatika kwa umeme kwa saa sita.
“Baada ya nyani huyo kufanikiwa kupenya na kuingia kwenye mitambo hiyo, alipigwa na shoti hiyo lakini cha ajabu ni kuwa hakufa. Alifanikiwa kupona lakini alikutwa na majeraha mengi, na kisha kukabidhiwa kwa idara ya wanyama pori,” alisema Kapata.
Aidha, Kapata alisema kuwa tatizo hilo limefanikiwa kutatuliwa na umeme sasa umerudi kwenye majimbo yote ya Kusini na Magharibi ambayo yalikumbwa na tatizo hilo.
“Angelikuwa ni binadamu ndiye aliyesababisha tatizo hilo na hakufa, basi angekabiliwa na kifungo cha miaka 10 hadi 25 jela,” alisema Kapata.
BBC

No comments

Powered by Blogger.