Wasiwasi wa abiria wairudisha ndege ya Air Asia X ilikotoka

BRISBANE- NDEGE
ya kampuni ya Air Asia X iliyokuwa ikielekea Kuala Lumpur, Malaysia,
ililazimika kurudi nchini baada ya ndege wawili walioingia kwenye injini kuwatia
wasiwasi abiria.
Ndege hiyo
iliyokuwa na abiria 359, ilipata matatizo baada ya kupaa siku ya Jumatatu. Abiria
waliripoti kusikia kelele kubwa na kuona miale ya moto ikitoka katika mashine
ya ndege hiyo, kabla ya kutua salama mjini hapa saa moja baadaye.
Mabaki ya
ndege wawili yalipatikana katika barabara ya ndege hiyo, kulingana na kampuni
hiyo. Abiria mmoja, Tim Joga aliliambia jarida la asubuhi la Morning Herald
kuwa, alihisi milio minne ya kelele kati ya mitano na mwanga mwingi.
Abiria
mwengine, Eric Lim alisema kuwa kisa hicho kilitokea muda mfupi baada ya ndege
hiyo kupaa.
“Kulikuwa na
miale ya moto na sauti za boom boom boom na watu wakaanza kulia na kusema ‘Mungu
wangu, Mungu wangu,” Lim aliandika katika ukurasa wake kwenye mtandao wa Facebook.
Mkurugenzi
wa kampuni ya Air Asia X, Benyamin Ismail alisema kuwa rubani na wafanyakazi wa
ndege walichukua hatua ya kuwahakikishia usalama abiria wakati wa kisa hicho.
“Air Asia X
sasa itapanga ndege maalum ya kuwasafirisha wageni wote katika ndege D7 207
inayoelekea Kuala Kumpur haraka iwezekanavyo,” alisema Ismail katika taarifa
yake.
Wiki
iliopita ndege ya Air Asia X, ililazimika kurudi Perth baada ya tatizo la
mashine kuifanya itetemeka ‘kama mashine ya kuosha nguo’. Mapema mwezi huu,
ndege ya China Eastern Airline ilitua kwa ghafla mjini Sidney baada ya shimo
kubwa kuonekana katika mashine yake.
Desemba 2014,
ndege ya Air Asia ilianguka katika bahari ya Java na kuwaua abiria 162, baada
ya mfumo wa rada wa ndege hiyo kutofanya kazi ilipokuwa angani.
BBC
No comments