Header Ads

‘Wanariadha wa kike wenye homoni za kiume wana uwezo mkubwa kuliko wenzao’



Mwanariadha wa mita 800 kutoka Afrika Kusini Caster Semenya
Caster Semenya. Mwanariadha huyu wa Afrika Kusini, ni mmoja kati ya wanariadha wanaodaiwa kuwa na homoni nyingi za kiume kiasi cha wengi kudhani kuwa ni mwanaume na si mwanamke.
LONDON- UTAFITI mpya unasema kuwa wanawake wanaozaliwa na viwango vya juu vya homoni za kiume (Testosterone), wana uwezo mkubwa wa utendaji ikilinganishwa na wenzao katika mashindano.

Hata hivyo, watafiti hao wamebainisha kwamba ushirikiano kati ya viwango vya juu vya homoni za testosterone na utendaji bora, haufai kuchukuliwa kama thibitisho.
Ripoti hiyo iliyochapishwa katika jarida la matibabu katika michezo, inatokana na sampuli 100 za damu zilizochukuliwa kutoka kwa wanariadha katika kipindi cha miaka miwili.
Kuja kwa ripoti hiyo ambayo imechapishwa wiki chache kabla ya Mahakama ya Usuluhishi kuhusu masuala ya michezo, kutoa uamuzi wake wa mwisho kuhusu uamuzi wa shirikisho la wanariadha duniani I.A.A.F kuwapiga marufuku wanariadha wa kike walio na homoni nyingi za kiume.
Marufuku hiyo iliyoanzishwa 2011, ilisitishwa na mahakama hiyo miaka miwili iliopita.
BBC

No comments

Powered by Blogger.