Header Ads

Wanne mbaroni kwa mauaji ya watu wenye vipara Msumbiji



mauaji ya watu wenye vipara
MAPUTO- POLISI katika jimbo la Zambezia nchini, wamewakamata watu wanne kwa madai ya kuhusika na mauaji ya watu wenye vipara.

Wamesema wanaendelea pia na uchunguzi kuhusiana na mauaji hayo, huku wakifuatilia zaidi kujua nani anachochea mauaji hayo.
Waganga wa kienyeji wamekuwa wakidaiwa kusambaza habari zisizo na ukweli, kwamba vichwa vya watu wenye vipara vina dhahabu ndani.
Pi, Polisi wamekuwa wakichunguza mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) ambao wanakatwa viungo vyao vya mwili, na kutumika katika masuala ya imani za kishirikina.
Aidha, wamesema washukiwa hao wa mauaji wanatoka katika nchi jirani.
BBC

No comments

Powered by Blogger.