Header Ads

Wapalestina wapinga hatua mpya za Israel



Graphic showing Temple Mount/Haram al-Sharif

JERUSALEM- KIONGOZI wa Palestina, Mahmoud Abbas anasema kuwa ataendelea kukata mawasiliano na Israeli licha ya kuondolewa kwa mitambo ya kutambua chuma katika eneo Takatifu Mashariki mwa Jerusalem.
Kuwekwa kwa mitambo hiyo, kulisabaisha ghasia mbaya na Wapalestina ambao waliiona kama hatua ya Israel kutaka kudhidti eneo hilo. Israel ilisema kuwa, ilikuwa muhimu kuzuia silaha kuingizwa eneo hilo. Inasema sasa ina mipango ya kuweka kamara za ulinzi.
Pande zote ziko chini ya shinikizo kutoka jamii ya kimataifa kutatua mzozo huo, katika eneo hilo takatifu ambalo kwa waislamu linajulikana kama Haram al-Sharif na kwa wayahudi kama Temple Mount.
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa eneo la Mashariki ya Kati, ametaka misukosuko kupungua kabla ya maombi ya Ijumaa ambayo huhudhuriwa na maefu ya watu. Hatua mpya za usalama, zilichukuliwa kufuatia kuuliwa kwa polisi wawili wa Israel.
Licha ya kuongezeka kwa misukusuko, ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, ilisema jana kuwa itaondoa mitambo ya kutambua chuma na kuweka teknolojia tofauti iliyo bora.
Hatua mpya zitawekwa ndani ya kipindi cha miezi sita inayokuja, huku polisi zaidi wakiwekwa hadi wakati huo. Kulingana na shirika la habari la Reuters, watu walionekana wakiondoa mitambo hiyo na kamera zilizowekwa juzi.
Lakini Rais Abbas na kiongozi wa Kiislamu ambaye anasimamia eneo hilo takatifu, walitupilia mbali mabadiliko hao wakitaka hali kurejea kawaida.
BBC.

No comments

Powered by Blogger.