Header Ads

Aliyefanya shambulizi kwa msumeno akamatwa Uswisi



Franz Wrousis hajaeleza kwanini alifanya tukio hilo

GENEVA- POLISI nchini, wamasema wamemkamata mtu mmoja aliyetambuliwa kama, Franz Wrouisis ambaye anaaminika kufanya shambulizi la kuwajeruhi watu kwa kutumia msumeno mwanzoni mwa wiki.
Shambulizi hilo lilifanywa ndani ya ofisi moja ya umma Jumatatu ya wiki hii katika mji wa Schaffhausen. Baada ya tukio hilo, Wrousis mwenye miaka 51 alimakatwa kilomita 60 nje ya mji huo ambako alitekeleza shambulizi hilo.
Wafanyakazi watano kwenye ofisi hiyo inayohusika na masuala ya bima ya afya, walijeruhiwa vibaya huku mmoja hali yake ikisemekana kuwa ni mbaya zaidi.
Mshukiwa huyo alikuwa akifuatiliwa na polisi kabla ya tukio hilo. 
BBC.

No comments

Powered by Blogger.