Korea Kaskazini yarusha kombora kwenye bahari ya Japan

SEOUL- Korea
Kaskazini imerusha kombora jingine la masafa marefu, kutoka jimbo lake la Magharibi
kulingana na mamlaka za Japan na Korea Kusini.
Kombora hilo
lilirushwa kutoka mji wa Bangyon, Kaskazini mwa mkoa wa Pyongyang kulingana na
chombo cha habari cha Yonhap kikitaja duru za Jeshi la Korea Kusini.
Japan,
imesema kuwa kombora hilo huenda lilianguka katika eneo la kiuchumi la bahari
ya Japan. Korea Kaskazini imeongeza viwango vya majaribio vya makombora yake
katika meizi ya hivi karibuni, hatua inayoendelea kuzua wasiwasi.
Kombora hilo
la jana lilisafiri umbali wa kilomita 930 kwa dakika 40, kulingana na Korea
Kusini na Japan. Hili ni kombora la 11 lililogunduliwa mwaka huu, lakini urefu
wake umeongezeka kulingana na mwandishi wa BBC mjini Seoul, Stephens Evans.
Mara ya
mwisho, Korea Kaskazini ilifanyia majaribio kombora lake mwezi uliopita. Ilirusha
makombora yake katika wakati tofauti, yote yakielekezwa bahari ya Japan.
Waziri wa
Mambo ya Ndani nchini Japan, Yoshihide Suga aliwaambia waandishi wa habari
kwamba; “Uchokozi kama huu wa Korea Kaskazini hauwezi kukubalika. Tuliwasilisha
malalamishi yetu na kushutumu hatua hiyo.”
Rais mpya wa
Korea Kusini aliyechaguliwa hivi karibuni, Moon Jae-in ametaka kufanywa kwa
mkutano wa dharura katika Baraza la Usalama la Taifa hilo.
Moon pia
alikutana na Rais wa Marekani, Donald Trump wiki iliyopita, huku kiongozi huyo wa
Marekani akiionya Pyongyang kwamba itapata jibu sahihi.
Kurushwa kwa
kombora hilo kunajiri siku moja, baada Rais Trump kuzungumza kwa simu na Waziri
Mkuu wa Japan, Shinzo Abe na Rais wa China, Xi Jinping kuhusu Korea Kaskazini.
Viongozi hao
walithibitisha jitihada zao za kuhakikisha kuwa hakuna utumizi wa nyuklia
katika rais ya Korea.
No comments